50 views 3 mins 0 comments

BARABARA KUFUNGWA DAR,BODABODA,BAJAJI HAZIRUHUSIWI MJINI

In KITAIFA
January 27, 2025

Na Mwandishi Wetu WAMACHINGA

– Asema mpaka sasa Marais wengi wamekwishafika

– Kufuatia uwepo wa ugeni huu Mkubwa baadhi ya barabara zitafungwa na kufunguliwa ili kuepusha usumbufu kwa wageni

– Asisitiza kuwa Serikali imeelekeza tarehe 27-28 Januari, 2025  Watumishi wa Umma Dsm kufanyia kazi Nyumbani

– Agusia suala  la Usafi, Ulinzi na Usalama wa Mkoa wa Dar es Salaam

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila Leo tarehe 27 Januari, 2025 ametoa taarifa kwa Umma kupitia Waandishi wa Habari kuhusu Ujio wa Marais wanaotoka katika Mataifa ya Afrika kuhudhuria Mkutano wa Nishati tarehe 27-28 Januari, 2025 hapa Jijini  Dar es Salaam

RC Chalamila amesema mpaka sasa Marais wengi kutoka Mataifa mbalimbali wamekwishafika aidha hoteli zenye hadhi kubwa zimekwishajaa na inaonyesha kuwa Rais Samia ameuandaa Mkutano huo kwa Viwango Vikubwa vya Kimataifa

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa Ameeleza kuwa kufuatia kuwepo kwa ugeni huu Mkubwa baadhi ya barabara zitafungwa ili kuepusha usumbufu kwa wageni kama ilivyotangazwa na Jeshi la Polisi na msisitizo zaidi ni kuendelea kuvipunguza zaidi vyombo vya usafiri kupita kwenye zile njia ambazo zinaweza kuleta usumbufu Mkubwa kwa wageni wetu

Vile vile Mhe. Chalamila Amesisitiza kuwa *Serikali* imeelekeza tarehe 27-28 Januari 2025 Watumishi wa Umma Dar es Salaam  kufanyia kazi Nyumbani isipokuwa wale ambao mazingira yao ya kazi yanawataka kuwepo katika Vituo vyao vya kazi kama vile Watumishi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama, Sekta ya Afya, Sekta ya Usafiri na Usafirishaji, Benki, Biashara Kariakoo, Hoteli na Migahawa aidhaa, Waajiri katika Sekta binafsi wanashauriwa kuruhusu Watumishi wao katika Mkoa wa Dar es Salaam kufanyia kazi Nyumbani au kuweka utaratibu ambao hautasababisha changamoto ya Usafiri  kutokana na kufungwa kwa Barabara hizo

Mkuu wa Mkoa Amegusia Suala la Usafi kuwa unaendelea kufanyika katika maeneo yote na hali ya Ulinzi na Usalama ni nzuri kama taarifa ilivyotolewa na Jeshi la Polisi na Vyombo vya Dola hata hivyo baadhi ya njia Kuna magari mengi ya Polisi na Vyombo vya Dola  hivyo kuwaasa wananchi wasiogope kwa sababu vyombo hivyo vinalenga kuhakikisha wageni pamoja na wenyeji wanakuwa *Salama* wakati wote

*Ikumbukwe kuwa Rais Samia anawatakia Watanzania wote na haswa wa Dar es Salaam kuendelea kuwa sehemu ya ukalimu kwa wageni wetu wanaokuja kuhudhuria Mkutano huo Mkubwa na  utarushwa mubashara kwenye vyombo mbalimbali vya habari ili Watanzani waweze  kuelewa azma kubwa na heshima ambayo Taifa letu limepewa la kuwa mwenyeji wa mkutano huo ambao unatarajiwa kuhudhuriwa na Marais wengi wa AFRIKA*

/ Published posts: 1715

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram