24 views 2 secs 0 comments

WATUMISHI WANAOPANDA MADALAJA KUJIEPUSHA NA RUSHWA

In KITAIFA
March 03, 2025

Na Madina Mohammed DODOMA WAMACHINGA





Katika mwaka wa fedha 2024/25 serikali inatarajia kupandisha vyeo watumishi  laki mbili kumi na tisa na arobaini na mbili (219042)na kubadilisha kada watumishi elfu sita Mia tisa na kumi (6910).

Haya yameelezwa  leo 3 march jijini Dodoma, waziri wa nchi ,ofisi ya Rais Utumishi na Utawala bora George  Simbachawene  katika kikao chake na wakuu wa Taasisi za umma.



Waziri Simbachawene ,amewataka watumishi wa umma  kuzingatia maadili ya kazi kwani kumekuwa na malalamiko kuhusu vitendo vya uvunjifu wa maadili ikiwemo Rushwa, ulevi kazini ,matumizi ya lugha zisizofaa na kugushibarua za uhamisho.

Hata hivyo jukumu la waajiri wa watumishi wa umma  ni kuendelea kuwasimamia watumishi waliochini yao kwa kuwa elimisha kuhusu haki na wajibu  wao ili wanapodai haki wajue kuwa ni wajibu wanapaswa kutekeleza.

/ Published posts: 1837

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram