
Na Mohamed Akida
ALIYEKUWA kipa namba moja wa Simba, Aishi Manula inaarifiwa yupo katika hatua za mwisho kujiunga na waajiri wake wa zamani Azam FC kwa ajili ya kuitumiki a msimu ujao.
Kipa huyo aliyekosa nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha Simba mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu na hakuna maongezi ya mkataba mpya.
Taarifa za kuaminika kutoka ndani ya uongozi wa Azam FC zinaeleza kuwa wapo katika hatua za mwisho kumalizana naye na anaamini msimu ujao ataitumikia Azam FC.
“Nikwli tulikuwa katika mazungumzo na Manula kuona kama anawza kurejea nyumbani msimu ujao siwzi kusema hohote kwa sasa lakini mazungumzo yetu yanakwena vizuri,” Kimeeleza chanzo hicho.
Kiongozi huyo ameelza kuwa nao ili hilo litakamilika wanamini eno lao la makia litakuwa limeimarika kwa kiasi kikubwa kutokana na kujaribu mkia wengi siku za karibuni bila mafanikio.
Kabla ya kwena Simba alikohuumu kwa misimu saba, Manula aliibukia Azam FC, timu ambayo aliichezea kwa mafanikio makubwa ikiwemo kuipa taji la Ligi Kuu msimu wa 2013\14.