12 views 2 mins 0 comments

MUSICHOCHEE VURUGU TANZANIA YETU NI YA AMANI-AHMED KOMBO

In KITAIFA
May 25, 2025

Na Mwandishi Wetu WAMACHINGA

Baadhi ya Wanaharakati nchini Tanzania  wametoa  rai kwa vijana  wa kenya  ambao wanaendelea kumkebehi na kumtukana   Rais DKt Samia suluhu Hassani   na kuchochea  vurugu   na Vitendo  vya uchochezi nchini.


Hayo yamesemwa jijini Dar es salaam na Mwanaharakati Ahmedi kombo  mara baada ya kuzungumza na Wanahabari  ambapo ametoa rai kwa baadhi ya vijana  kutoka kenya kuacha kufanya Vitendo vya  uchochezi nchini kwetu Tanzania kwani wanaharibu sifa za nchi yetu na viongozi kwa ujumla wakati huku Rais huyo huyo anaendelea kujenga Maendeleo mbambali ya nchi katika kujikwamua kiuchumi.


“Sisi kama vijana wazalendo tumeona tutoe tamko kwa kile kinachoendelea  Tanzania  hatutokubali mtu yeyote aweze kuvuruga na  kuharibu amani ya nchi yetu pia kuna mwanasiasa kutoka kenya  Martha karua naye anaungana na baadhi ya watanzania kusema baadhi ya viongozi wetu aendelee na shughuli nyingine nchini kwake atuachie nchi yetu. “Amesema kombo”



Aidha tutaendelea kukemea Vitendo hivi katika kipindi hiki tunachoenda kwenye uchaguzi mkuu hivyo kwa sasa nchi yetu iko salama katika Vitendo hivyo vya uhalifu huku jeshi la polisi likiendelea kulinda  Ulinzi na usalama wa Raia.



Vilevile Kuna Mitandao ya kijamii inatumia kupotosha watu pasipo na ukweli wowote na kutoa taarifa ambazo sio sahihi hivyo kwani viongozi wetu wanajitahidi kulinda Wananchi wake nyakati zake



Mwanaharakati wa siasa Joseph Yona Amesema kuwa kuna chama pinzani bado kinaendelea na uchochezi wa kisiasa kwa kutumia watu kadhaa  na kuharibu sifa za viongozi wetu nchini sisi kama wanaharakati hatutokubali kuwachafua viongozi wetu kwa namna yeyote ile tutaendelea kukemea vikali.

Nchi  yetu ina Amani hivyo kuna Watu wachache akiwemo Maria Sarungi na kundi lake kutaka kuifanya Tanzania Sehemu ya vita  tunatoa wito kuwa Nchi yetu haihitaji vita wala mapigano tunahitaji Amani tu sio vinginevyo “Amesema Joseph Yona”

/ Published posts: 2108

Ukurusa rasmi wa gazeti la Wamachinga. #sautiyawanyonge

Twitter
Youtube
Instagram